Wanandoa
wametakiwa kuepuka migogoro ya kifamilia ambayo ndiyo inawathiri watoto wao na kupelekea
kukimbia majumbani makwao na Kwenda mitaani kisha kulelewa kama watoto wenye
Uhitaji.
Hayo
yamesemwa na Mwenyekiti wa Kundi la Friends Of Batuli Bwana Yesaya Mkwaju wakati
walipotembea kutoa msaada kituo cha watoto wenye uhitaji Cha Kindness Children
Care Orphanage Cente ambacho kinalea watoto wenye uhitaji kilichopo Eneo la
Kijenge kata ya Mushono halmashauri ya Jiji la Arusha.
Mkwaju
amesema kuwa tangu kuanza mwaka huu wa 2018 wameshatembelea vituo vitatu na
kutoa misaada Mbalimbali wao kama kauli mbiu yao inavyosema Saidia Jamii yako Kadri Ulivyobarikiwa huku
akiwataka watu mbalimbali kuendelea kujitokeza kusaidia watoto wenye uhitaji.
Kwa
upande wa afisa ustawi wa jamii kutoka jiji la Arusha Bi Nivoneia Kikaho ambaye
aliongozana na Kundi Hilo la Friends Of Batuli kwenda kutoa misaada katika
kituo hicho cha Kindness amesema kuwa mifarakano ya Ndoa pamoja na Ugonjwa wa
Ukimwi imekuwa sababu ya Kuongezeka kwa watoto wenye Uhitaji.
Naye
Mlezi wa Kituo Hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Kituo Hicho cha Kindnes Children
care Mchunaji Yohana Mwampamba amesema kuwa wanaume kukwepa majukumu yao katika
familia na kuwaachia wanawake peke yao Pia imepelekea kuwepo kwa watoto wenye
mahitaji
Hata
hivyo Kundi la Friends Of batuli limekuwa na Desturi ya kutoa misaada
mbalimbali kwa jamii yenye uhitaji ambapo leo katika kito hicho wametoa vyakula
kwa ajili ya kusaidia watoto hao.
Migogoro ya Kifamilia na Changamoto za Kimaisha vyapelekea kuongezeka kwa Watoto Wenye Uhitaji
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 29, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment