MADIWANI wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, ambao walitangazwa kuvuliwa uanachama,
wamewasilisha rasmi barua za kujiuzulu nafasi zao kwa Mkurugenzi wa Jiji hilo
Madiwani hao ni wale walidaiwa kukaidi maagizo ya viongozi
wa chama hicho kuhusu mwaliko wa Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson, wa kwenda
bungeni jijini Dodoma
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Dk. Amani Kilemile,
aliwataja madiwani hao na kata zao kuwa ni Geofrey Kajigili (Sisimba), Newton
Mwatujobe (Manga), Mchungaji David Ngogo (Nsalaga) na Humphrey Ngalawa (Iwambi
Dk. Kilemile alisema madiwani hao walianza kuwasilisha barua
zao kuanzia Julai 18, mwaka huu, na kwamba diwani wa mwisho aliwasilisha Julai
25
“Kutokana na madiwani hawa kuwasilisha barua zao, natangaza
rasmi kuwa kuanzia sasa si wajumbe wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri yetu ya
Jiji la Mbeya,” alisema Dk. Kilemile
Alisema baada ya kupokea barua hizo, amechukua hatua
mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumwarifu Mstahiki Meya wa Jiji hilo, David
Mwashilindi, kuhusu kujiuzulu kwa madiwani hao
Alisema kwa mujibu wa sheria za uchaguzi, mstahiki meya
anatakiwa kuwasilisha taarifa ya kujiuzulu kwa madiwani hao kwa Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa hatua zaidi na barua tayari
imeandaliwa, kilichobaki ni kutiwa saini na kutumwa
Aidha, alisema kwenye barua zao, madiwani hao wameeleza
sababu zinazofanana za kujiuzulu kuwa ni kutoelewana na viongozi wa chama chao
na kwamba wananyanyaswa wakidaiwa kuwa ni wasaliti
Alisema madiwani hao wameeleza kwenye barua zao kuwa
wameingia kwenye mgogoro na viongozi wao kutokana na kushirikiana na wadau
mbalimbali wa maendeleo katika Jiji hilo
Julai 21, mwaka huu, uongozi wa Chadema Wilaya ya Mbeya
Mjini, chini ya Mwenyekiti wake, Obadiah Mwaipalu, ulitangaza kupeleka
mapendekezo katika ofisi ya chama hicho Kanda ya Nyasa kuwafuta uanachama
madiwani watatu
Madiwani waliopendekezwa na chama hicho kufukuzwa ni
Kajigili, Mwatujobe na Ngallawa, ambao walidaiwa kukiuka katazo halali la
chama hicho la kutohudhuria mwaliko wa Naibu Spika, Dk. Tulia Akson, bungeni
jijini Dodoma
Aidha, siku hiyo hiyo, Ngogo alitangaza kujivua udiwani na
uanachama wa Chadema kwa kile alichodai kuandamwa na viongozi wa chama hicho baada
ya kuungana na Naibu Spika kwenye shughuli za maendeleo
Hata hivyo kabla uongozi wa chama hicho haujatoa uamuzi
wake, madiwani hao wameamua kuandika barua za kujiuzulu.
Madiwani walioponzwa na naibu spika kujiuzulu kujiunga na CCM
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment