CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesikitishwa
kuibuka michango mbalimbali kwa shule za msingi na sekondari kwa kuwa
serikali ilitangaza kuifuta.
Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema alisema
hivi sasa baadhi ya wananchi katika maeneo mbalimbali mkoani humo
wanachangishwa kiasi cha Sh. 10,000
Lema aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa
kampeni za uchaguzi mdogo katika Kata ya Mawenzi iliyopo Manispaa ya Moshi,
wakati akimnadi mgombea udiwani wa chama hicho, Afrikana Mlay
Alisema anashangazwa na kitendo cha serikali kutangaza kutoa
elimu bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na tayari kumeanza
kujitokeza changamoto hiyo
Alisema changamoto anayoiona ni CCM kunakili sera za
Chadema, licha ya kujipambanua wanaweza kuzitekeleza lakini inaonekana kama
mpango huo unataka kuwashinda.
Aidha, Lema alisema Chadema kinatoa angalizo kwa
wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga) juu ya zoezi la kutengenezewa
vitambulisho kwa Sh. 10,000 zoezi hilo limeghubikwa na utata mkubwa na
linalenga kuwatambua na kuwalipisha kodi kubwa
Alisema Chadema hawapingi zoezi la kuwatambua machinga na
kuwapatia vitambulisho kwani inatambua ili wananchi waweze kupata huduma za
afya ,ujenzi wa barabara na upatikanaji wa huduma za maji ni lazima
wananchi walipe kodi
Alisema kabla ya Machinga kutakiwa kulipia vitambulisho kwa
Sh. 10,000 serikali ilipaswa kuwaelimisha na kuwapatia mtaji pamoja na maeneo
maalumu kwa ajili ya kufanyia biashara zao kwa uhakika na usalama
“Hivi vitambulisho mnavyoaandaliwa mjiandae kutambulika
mjulikane ni akina nani na mpo wangapi ili muweze kulipishwa kodi hii inapaswa
kutazamwa kwa jicho la ziada ili kuweza kuwasaidia machainga kuondokana na
kunyanyasika katika nchi yao”alisema Lema
Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Killimanjaro,
Grace Kiwelu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake (Bawacha) alisema
Chadema kimejipanga kunyakua ushindi wa kishindo kata za Makanya Same na kata
ya Mawenzi mjini Moshi.
Alisema wananchi hawana budi kuondoa hofu ya
kushindwa katika uchaguzi mdogo wa marudio ya udiwani na ubunge kwa kuwa chama
hicho kimejipanga kulinda kura zao kwa gharama yoyote kwani wanachama na
baadhi ya wananchi wamekuwa na hofu ya kuporwa ushindi wao katika marudio ya
uchaguzi ndogo zinazoendelea hapa nchini.
Kiwelu alisema baraza la wanawake chadema na vijana mkoa
Kilimanjaro watahakikisha wanalinda kura zao zote na hakuna mtu atakayeweza
kupora ushindi wa umma na kubadilisha matokeo huku akitoa rai kwa tume ya
uchaguzi na serikali kuhakikisha zoezi la marudio ya uchaguzi mdogo linafanyika
na linamalizika kwa uhuru na amani
Kiwelu alisema tume ya uchaguzi haina budi kuhakikisha zoezi
hilo linafanyika kwa kufuta sheria kanuni na maadili yaliyowekwa na serikali na
vyama vya siasa ili zoezi hilo liweze kumalizika kwa amani na
kuwachukulia sheria kali wale wote watakaobainika kuvunja sheria za uchaguzi
Chadema walia michango kwa Shule za Msingi ,Sekondari
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment