Jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia madereva wawili
wa kampuni ya mabasi ya King Msukuma kwa makosa ya kuendesha magari yakiwa
mabovu na kuhatarisha usalama wa abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Mwanza
kwenda Kagera na jingine likitokea Kagera kwenda Mwanza
Ubovu wa magari hayo ulisababisha abiria 120 kulazimika
kulala kwenye kituo kikuu cha polisi Geita hadi walipoletewa usafiri mwingine
jana asubuhi na kuendelea na safari zao
Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 3, Kamanda wa
polisi mkoani hapa Mponjoli Mwabulambo amesema magari hayo yalikamatwa jana saa
11 jioni katika operesheni ya ukaguzi wa magari inayoendelea mkoani hapa
Mponjoli amesema katika operesheni waliyoifanya walikagua
magari 59 na 47 yalikutwa na makosa madogomadogo na kutozwa faini, mawili
yalikuwa na matatizo makubwa na kuzuiwa kuondoka huku mengine yakiruhusiwa
kuendelea na safari baada ya kuonekana hayana tatizo
Amesema madereva wa mabasi ya kampuni ya King Msukuma
wanaoshikiliwa ni Kini Daud (50) na Omary Oloyce
Madereva wawili mabasi ya King Msukuma watiwa mbaroni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment