Abiria zaidi
ya 120 waliokuwa wakisafiri na magari mawili ya kampuni ya King Msukuma
walilazimika kulala kituo cha Polisi jana Julai 2 baada ya kukamatwa na Polisi
wa usalama barabarani kutokana na ubovu
Magari hayo
yalikamatwa jana saa 11 jioni yakiwa safarini kutoka Mwanza kwenda Kagera na
jingine kutoka Kagera kwenda Mwanza
Akizungumza na
waandishi wa habari leo Julai 3, kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Mponjoli
Mwabulambo amesema magari hayo
yamekamatwa katika operesheni inayoendelea ya
ukaguzi wa magari yanayoingia na kutoka katika kituo kikuu cha magari mjini
Geita
Kamanda
Mwabulambo amesema katika operesheni waliyofanya jana magari 59 yalikaguliwa na
47 yalikutwa na makosa madogo na kutozwa faini
Amesema magari
mawili ndiyo yaliyokamatwa na kuzuiwa lakini leo asubuhi walipakiwa kwenye
magari mengine na kuendelea na safari zao.
Abiria 120 walala kituo cha polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment