Madiwani wageuka 'mbogo' mbele ya Mkurugenzi

Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Handeni wametishia kumchukulia hatua Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kutokana na kupata hati yenye mashaka. 

Hayo yamejiri wakati wa kikao maalum cha kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha  2016 hadi 2017 ambapo halmashauri ya wilaya ya Handeni imepata hati yenye mashaka jambo lililoacha baadhi ya madiwani kutokuwa na imani na mkurugenzi wao.

Hata hivyo mkurugenzi katika kuhakikisha hapotezi kibarua chake amesema kuwa kuanzia sasa ataanza kuchukua hatua kwa wakuu wa idara waliohusika na upatikanaji wa hati hiyo inayotia mashaka.

Kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shighela nae akawaunga mkono madiwani hao kwa kusema kuwa wasiwaonee haya watumishi ambao wamekuwa chanzo cha halmashauri hiyo kupata hati chafu.

Madiwani wageuka 'mbogo' mbele ya Mkurugenzi Madiwani wageuka 'mbogo' mbele ya Mkurugenzi Reviewed by KUSAGANEWS on July 03, 2018 Rating: 5

No comments: