Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema hatasita
kufuta makanisa au misikiti inayoshindwa kutatua migogoro ya taasisi hizo
Ametoa kauli hiyo leo katika Kanisa la Pentekoste la
Leganga, lililopo Arumeru mkoani Arusha Ambapo Amesema Kuanzia sasa, kanisa
lolote au msikiti wowote utakaokumbwa na migogoro na kushindwa kuitatua
wenyewe; misikiti hiyo, makanisa hayo nitakwenda kuyafuta mara moja
Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha yanakuwapo makanisa
na misikiti inayohubiri amani na utulivu.
Waziri Lugola ameonya askari Polisi wanaowashusha jukwaani
masheikh na wachungaji inapofika saa 12:00 jioni, akisema muda huo ukifika
waimarishe ulinzi ili waumini wamalize ibada zao vizuri
Lugola atishia kufuta makanisa, misikiti yenye migogoro
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 29, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 29, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment