Lugola amuondoa mjumbe wa polisi


Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemuondoa katika ujumbe wa Sekretarieti ya Kuzuia Biashara Haramu ya Binadamu, 

Abubakar Yunusi ambaye ni Inspekta wa Polisi Kitengo cha Uhamiaji
Lugola amechukua uamuzi huo leo Julai 30, 2018 baada ya Yunusi kusema kuna vyombo vilivyotumika kusafirisha binadamu vimekamatwa na vinasubiri kutaifishwa, lakini hana takwimu

"Wewe umejitambulisha mjumbe wa kamati ya kudhibiti usafirishwaji haramu wa binadamu, umesema kuna vyombo vimetumika, huna idadi yake. Unafanya kazi ya ubabaishaji hapa? Huwezi kuja kwenye maonyesho hujui idadi yake. Kazi yako ya ujumbe hakuna," amesema

Lugola alikuwa akikagua mabanda ya maonyesho katika Viwanja vya Mnazi Mmoja yanakofanyika maadhimisho ya kupinga usafirishaji wa bindamu
Lugola amuondoa mjumbe wa polisi Lugola amuondoa mjumbe wa polisi Reviewed by KUSAGANEWS on July 30, 2018 Rating: 5

No comments: