"Kundi la Friends Of Batuli litakuwa Hazina ya Arusha na Tanzania ,Mengine yaige "Dkt Kihamia Mkurugenzi wa Nec


Aliyekuwa Mkurugenzi Wa Jiji LA Arusha ,Athumani Kihamia, ameeleza kuyatambua makundi Mbalimbali yanayofanya kazi za kijamii katika jiji Arusha likiwemo kundi  la Friends Of Batuli kwa kuwa yamekuwa msaada  Mkubwa kwa wananchi hasa kwa kuwa kwamua na maisha Magumu.
 
Akizungumza na Kusaganews kwa njia simu katiika mahojiano maalum Kihamia amesema analikubali  kundi hilo la Friends of Batuli lenye Makao yake Makuu  Jijini Arusha amelisifu Kundi hilo kwa kuwa linakuja juu na linafanyakazi zake kwa mujibu Wa sheria na taratibu za nchini.

Amesema yeye ataendelea kutoa mchango wake kwa kundi Hilo kwa kuwa limekuwa hazina kwa jiji la Arusha Pamoja na Nchi kwa ujumla
Awali Kihamia ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi Wa Tume ya uchaguzi Nchini (NEC) ametajwa kuyapa 
ushirikiano  makundi hayo wakati alipokuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha jambo lililosaidia kupunguza changamoto za watu wenye kuhitaji msaada wakiwemo watoto yatima

Moja ya Makundi hayo ni pamoja na Friends of Batuli linaloongozwa na Mwl.Batuli Kisaya ambapo Kihamia amedai kwamba kundi hilo linakuja vizuri tofauti na makundi mengine ambayo yamekuwa mstari wa mbele kujinufaisha 
Kihamia  ameomba kundi hilo  liungwe mkono kwa kuwa limekuwa la Mfano  kwa uchapa kazi Arusha

"Yapo Makundi Mengi ya kijamii katika jiji la Arusha  nayatambua ,ila hili kundi la Friends of Batuli linakuja  vizuri ni  miongoni mwa makundi ambayo ni hazina ya Arusha  ninachoshauri lipanue mipaka   zaidi na kufanyakazi na nje ya Arusha katika kuhudumia jamii''Amesema Kihamia

Aidha Kihamia  amewataka  watumishi Wa  halmashauri ya jiji la Arusha wakiwemo wakuu Wa idara kutoa ushirikiano Wa dhati  kwa Makundi ya kijamii yenye mrengo wa kuwanufaisha wananchi yanapokuwa yakitekeleza Majukumu yake

Ametoa wito kwa makundi mengine kuiga mfano Wa kundi la Friends of Batuli  na kuachana  na dhana ya kuendesha  makundi kwa lengo la kujinufaisha .
"Kundi la Friends Of Batuli litakuwa Hazina ya Arusha na Tanzania ,Mengine yaige "Dkt Kihamia Mkurugenzi wa Nec "Kundi la Friends Of Batuli litakuwa Hazina ya Arusha na Tanzania ,Mengine yaige  "Dkt Kihamia Mkurugenzi wa Nec Reviewed by KUSAGANEWS on July 31, 2018 Rating: 5

No comments: