Kukosekana kwa uzio katika kambi ya wazee wasiojiweza
wanaolelewa katika kituo cha Fungafunga kilichopo manispaa ya Morogoro
kumetajwa kuwa ni changamo kubwa inayo sababisha wazee hao kutoroka na kwenda
kuombaomba barabarani licha ya serikali kuwahudumia wazee hao kwa kila kitu
huku vibaka nao wakitumia nafasi hiyo kufanya udokozi wa mara kwa mara katika
kambi hiyo
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali
kutoka kwa kikundi cha umoja wa marafiki Kihonda (UMAKI ) mlezi wa wazee hao
Tehora Njimba pamoja na kuwashukuru wadau hao lakini pia amesema tatizo la
kukosekana kwa uzio ni changamoto kubwa kunako hatarisha ustawi na afya za
wazee hao
Kwaupande wao wazee hao wameomba serikali kuwapatia wataalamu
kupewa elimu ya ujasiamali ili waweze kuelimishwa kuhusiana na shughuli
mbalimbali ikiwemo ufugaji wa Kuku na bustani za Mboga huku mwenyekiti wa
kikundi cha UMAKI Peter Tarimo akieleza lengo la kikindi kuwatembelea wazee
hao.
Kukosekana kwa Uzio Kambi ya Fungafunga kwasababisha wazee Kutoroka
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment