Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Mhandisi Isaac
Kamwelwe, amewataka watendaji wa wakala wa ufundi na umeme nchini (TEMESA),
kujitathimi katika utendaji wao wa kazi kufuatia kuwepo kwa malalamiko mengi
kuhusiana na matengenezo ya magari ya serikali
Mhandisi Isaac Kamwelwe ametoa agizo hilo, wakati akipokea
rasmi kivuko kipya na cha kisasa cha MV. Mwanza kilichojengwa na mkandarasi
mzawa kampuni ya Songoro Marine ya Jijini Mwanza, ambacho kimegharimu shilingi
bilioni 8.9 za kitanzania, chenye uwezo wa kubeba abiria 1,000, tani 250
za mizigo na magari 36 kwa wakati mmoja ambacho kitatoa huduma ya usafirishaji
kati ya Kigongo - Busisi mkoani Mwanza ndani ya ziwa Victoria
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella pamoja na mkuu wa mkoa
wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, wamepongeza juhudi za rais John Magufuli za
kuboresha huduma za vivuko katika ziwa Victoria
Naye mwenyekiti wa bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali mstaafu
Mabula Mashauri amesema wakala huo utahakikisha miundombinu ya usafiri na
usafirishaji katika ziwa Victoria unakuwa bora, salama na wenye uhakika
Serikali yakabidhiwa cha Mv Mwanza
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment