Leo Jumapili Julai Mosi, 2018 saa 9 alasiri Katibu Mkuu
Kiongozi, Balozi John Kijazi alitangaza mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri
yaliyofanywa na Rais John Magufuli, huku Mwigulu Nchemba aliyekuwa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi akiachwa
Kabla ya kutangazwa kwa mabadiliko hayo, Mwigulu alikuwa
mkoani Kigoma katika ziara na leo saa 6:14 mchana alitembelea bandari ndogo ya
Kibirizi
Akiwa katika bandari hiyo, Mwigulu amesema Serikali ipo
tayari kuwarudisha makwao wakimbizi walio tayari
“Hakuna sababu ya kuwaacha wakimbizi kuendelea kukaa nchini
wakati wanahitaji kurudi makwao. Wapo wafadhili walio tayari kuwasaidia ili
wabaki nchini lakini wafadhili hawa wanapaswa kuielewa tu Serikali. Sasa
matatizo yamekwisha katika nchi zao hatuna sababu ya kuwazuia,” amesema
“Kwa wale wanaopenda kutunza wakimbizi waende nchi zenye
matatizo ambazo bado watu wanakimbia ila huku kwetu kwa wanaotaka kurudi kwao
lugha iwe moja ya kuwarudisha maana ndio sheria ya kimataifa inavyosema.”
Kazi ya mwisho ya Mwigulu akiwa waziri
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment