Kihamia nimepokea taarifa za uteuzi wa Mkurugenzi wa NEC nikiwa ndani ya Basi la Super Video Sikua najua
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Dokta Athumani Kihamia ambaye ameteuliwa hii leo Kuwa
mkurugenzi wa tume ya uchaguzi nchini Tanzania NEC amesafiri kwa kutumia basi la
kampuni ya Super Video linalofanya safari zake kutoka Dodoma mpaka Arusha
majira ya saa kumi ambapo taarifa za uteuzi amezipata akiwa ndani ya basi hilo.
Akizungumza kwa njia ya simu na Kusaga News Kihamia
Amesema kuwa akiwa ndani ya basi hilo kuja Arusha alipata meseji pamoja na simu
mbalimbali zikimpongeza kwa kuteuliwa huku akiwa hajui kinachoendelea lakini
wengi wao walikuwa wanampongeza na kumuambia Hongea Kihamia umeteuliwa kuwa
katibu mkuu wa NEC
Tulipomuuliza kwanini ametumia usafiri wa basi ile hali
ana gari ambalo ni maalum kwa ajili ya mkurugenzi amesema kuwa wakati mwingine
anachangamana na jamii kuona changamoto wanazokutana nazo pamoja na kuunga
mkono juhudi za Dokta Magufuli za kubana matumizi ili pia fedha hizo pia
zisaidie wananchi wa hali ya chini
"Leo niliamua kutumia usafiri wa basi kama wananchi wengine na hata sikujua kinachoendelea lakini kutokana na simu nyingi nilizopata ni kwamba nimepokea nikiwa ndani ya basi la Super Video la kutoka Dodoma kuja Arusha"Alisema Kihamia
Pia ameongeza kuwa siyo mara ya kwanza kutumia usafiri
wa basi ambapo hata watumishi wake wakati mwingine hutumia usafiri huo huo pale
inapowalazimu kushughulikia shughuli za wananchi hivyo kutoa wito kwa viongozi
wengine kutojisahau wanapokuwa katika magari yenye hadhi watumie siku moja moja
ili waone taabu pia wanazopata wananchi wa hali ya chini.
Kihamia alikuwa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kuhudhuria
semina za uchaguzi mdogo wa madiwani kwa kata ambazo ziko wazi madiwani wake
walijiuzulu hivyo kujiandaa kwa ajiliya marudio.
Hata hivyo Mkurugenzi Kihamia amemshukuru Raisi Dokta
Magufuli kwa kumteua na kumuona anafaa katika nafasi hiyo na ameahidi
kuitumikia vema


Kihamia nimepokea taarifa za uteuzi wa Mkurugenzi wa NEC nikiwa ndani ya Basi la Super Video Sikua najua
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment