Ikiwa imepita siku 1 tangu
ilipotokea ajali ya lori Jijini Mbeya katika mlima wa Igawilo na kusababisha
kuua mtu mmoja, Jeshi la Polisi mkoani humo limesema limeshafahamu kiini cha
ajali hizo za kila mara na kudai lina mikakati madhubuti ya kudhibiti eneo hilo
kwa kushirikiana na TANROADS.
Picha hii ni miongoni mwa ajali
zilizotokea katika mlima wa Igawilo siku za hivi karibuni na kusababisha kuua
takribani watu watano
Hayo yamebainishwa na Kamanda wa
Jeshi la Polisi mkoani humo, Ulrich Matei Amezungumza na kusema eneo hilo la mlima wa Igawilo wameshafanyia uchunguzi
wa kina kuhusiana na ajali zinazotokea mara kwa mara ambapo kwa sasa
wamejipanga kuweka ukaguzi wa magari yote kabla hayajafika katika mlima huo
pamoja na kuweka vibango vya barabara vitakavyokuwa vikitoa maelekezo husika
juu ya kuwepo mlima huo ili madereva wawe makini zaidi.
"Tumeshawasiliana na
Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ili kuhakikisha zile alama za barabarani
zinakuwepo na hadi dakika mimi mwenyewe nipo katika huu mlima ninaona wameshafunga
hizo alama za kuwajulisha madereva wote kuteremka taratibu ili wasipate
ajali", amesema Kamanda Matei.
Mbali na hilo, Kamanda Matei pia
ameeleza chanzo cha ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika mlima wa
Igawilo na kusema lori hilo lilikuwa limebeba mbao na kusababisha kuelemewa
wakati wa linataka kushuka mlima huo ndipo gari likaangukia upande mmoja huku
akisisitiza kuwa ajali hiyo haijasababishwa na kugongana na gari nyingine
yoyote ile.
"Ajali iliyotokea usiku wa
kuamkia leo ni ajali ya kawaida tu, maana lori hilo lilikuwa limebeba mzigo wa
mbao na kusababisha kulivuta gari pembeni na ndipo mzee mmoja aliyekuwepo ndani
ya gari hilo kutaka kuruka ili akimbie lakini gari hilo likamuegemea", amesisitiza Kamanda Matei.
Jeshi la Polisi yafungukia kiini cha ajali Mbeya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 09, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 09, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment