Jeshi la Polisi nchini
limetoa onyo kali kwa watu wanaofanya vitendo vya uhalifu katika bahari,
maziwa na mito mikubwa hapa nchini kuacha mara moja kwa kuwa
wamejipanga kuhakikisha wavuvi wana kuwa salama wakati wanapofanya
shughuli zao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi , IGP Simon Sirro akishuka kwenye chopa 'helicopter 'kufunga mafunzo ya Polisi wanamaji Mkoani Mwanza.
Kauli
hiyo imetolewa na IGP Simon Sirro Jijini Mwanza wakati wa ufungaji wa
mafunzo ya askari polisi wanamaji yaliyokuwa yakifanyika katika Chuo cha
Polisi Wanamaji kilichopo Jijini humo.
Aidha IGP Sirro amewataka wazazi kuwakanya watoto wao kutojihusisha
na vitendo vya uhalifu kwa kuwa serikali ya awamu ya tano haina mchezo
na wahalifu.
IGP Sirro yupo ziarani Mikoa ya Kanda ya Ziwa kukagua utendaji kazi
wa Polisi na kuzungumza na wananchi waishio katika visiwa ili kuimarisha
usalama hususani kwa wavuvi.
IGP Sirro atoa onyo kuhusu bahari
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 07, 2018
Rating: 5
No comments:
Post a Comment