Wananchi wa kata ya Pinyinyi na Ngarasero wilayani
Ngorongoro Mkoani Arusha wamempongeza Mbunge wa Jimbo hilo William Olenasha kwa
kuwatatulia changamoto ya Mtandao wa simu ambao kipindi cha nyuma walikuwa
hawawezi kuwasiliana kutokana na kukosekana kwa mtandao wa mawasiliano ya Simu.
Wakizungumza wakati wa mahojiano Maalum na Mwandishi wa
habari hii wananchi hao wamesema kitu cha kwanza ambacho kwasasa wanajivunia ni
kuwepo kwa uborsgaji wa mtandao wa simu ambao umekuja kutokana na Juhudi za
Mbunge wao
“Ni kweli mwandishi ukweli kabisa wakati wa miaka ya
nyuma tulikuwa ukitaka kupiga simu unaenda mpaka karatu au Mto wa mbu ambao ni
umbali mrefu sana kutoka hapa pinyinyi mpaka huko kwenda kupiga simu lakini
sasa hivi Mbunge wetu Olenasha ametuletea mtandao wa halotel sasa tunapiga
siunaona hata hapa niliposimama simu yangu Inaita kwahiyo oooi kwakweli sijui
huyu mbunge Mungu amsaidie na maisha marefu mana acha tu”Alisema Mwananchi
Akizungumza mmoja wa mwananchi aliyejitambulisha kwa
jina la Agnes Mollel amesema kuwa walikuwa hata biashara zao haziendelei
kwasababu walikuwa hawana mawasiliano yoyote ya kuwasiliana kata moja mpaka
kata nyingine lakini kwasasa wanapiga bila wasiwasi na Mbunge wao amewaahidi
kuendelea kuboresha huduma hizo za mawasiliano kuwa bora zaidi.
“Unajua kaka hakuna biashara inayoendelea mahali popote
bila kuwasiliana lakini sasa hivi nina uwezo wa kumpigia simu mtu kutoka Arusha
anitumie mzigo kwa Gari tu japo mtu hamjuani lakini Simu ndiyo kila kitu mimi
sitaki kumpamba mbunge wetu lakini Anafanya kazi nzuri ambayo kweli kila mtu
anaiona anapopita tuna mabarabara,maji,huduma za afya zinakuwa nzuri sasa yani
Olenasha nika Lulu ambayo tulikuwa tunaitafuta kwa muda mrefu sasa tumeipata
nayo sasa tunaona ina ng”aa kweli”Alisema Agnes
Naye mfanyabiashara ya Utalii katika eneo la Ngarasero
Heritenson Kiwale amesema kuwa amekuwa akifanya biashara ya watalii lakini
tatizo kubwa lilikuwa ni mawasiliano baina yao na watalii lakini kwasasa
wanawasiliana hata kama mtu uko ndani ya nyumba unaweza kupiga na kupokea simu
hivyo akawaomba wananchi kushirikiana kwa pamoja ili kuboresha zaidi
“Yani niseme labda mimi ni mfanyabiashara wa muda mrefu
sana yani labda Tangu uhuru hili eneo hakukuwa na kupiga simu wala kupokea
unatoka nayo mjini huko ukija inakaa tu kama kopo lakini sasa hivi nawasiliana
na mzungu yuko Canada kwa simu tu yani kweli kumendelea sana”
Kwa upande wa Mbunge William Olenasha amesema kuwa kwa
muda mrefu alipokuwa anaomba kura katika kijiji cha Pinyinyi changamoto kubwa
ilikuwa ni mtandao wa simu ambapo tayari anaendelea kuboresha zaidi na tayari
minara imejengwa na wananchi wanaendelea kupata maendeleo.
“Nimeshaleta minara miwili ambayo mmoja unafanya kazi
lakini mwingine unajengwa na umeanza wiki iliyopita katika mlima wa Kilai na halotel
wameniahidi ndani ya wiki mbili watakuwa wameuwasha na nitahakikisha kila
mahali panakuwa na network”Alisema Olenasha Mbunge
Jimbo la Ngorongoro Lenye kata 28 ambapo umbali wa
kutoka kata moja kwenda nyingine ni kiasi cha kilomita zaidi ya 25 lakini kama
Mbunge tayari ameshazunguka kata Zote lengo ni kuwasaidia wananchi wake
waliompigia kura na kumchagua ili awawaikilishe bungeni.
Wananchi wamuombea Mbunge wao kwa Mungu kwa kuwaletea mtandao wa Simu /Mawasiliano
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 07, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment