Zitto amshukia Kigwangalla


Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla kukubali amekosea na kurejea katika utaratibu wa awali wa utoaji wa vibali vya vitalu vya uwindaji

Akichangia bajeti ya wizara hiyo ya mwaka 2018/19 ambayo ni Sh115.8bilioni, Zitto amesema:, “Waziri kwa kuwa umeona kuna tatizo la kisheria na maagizo uliyoyatoa ni kinyume na sheria turejee katika utaratibu wa awali.”

Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa ACT-Wazalendo amesema hakuna anayepinga nchi kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme, “Lakini tunataka taratibu za sheria zifuatwe. Kitendo cha kukata miti zaidi ya 1,400 katika hifadhi ya Selous ukubwa sawa na jiji la  Dar es Salaam kweli, kila mbunge afumbe macho hapa aitizame Dar es Salaam isiyo na miti.”

“Lengo la wizara ifikapo mwaka 2025 ni nchi kuwa na watalii milioni nane kwa mwaka na kuingiza dola bilioni 16 za Marekani, ukienda kuiondoa selous yote huwezi kuifikia huku?”

Huku akizungumzia uzalishaji wa umeme wa gesi ulivyo gharama amesema, “Lakini kuzalisha kwa maji inatuchukua muda, suala la TFS (Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania) kwenda kuangusha miti si sahihi. Jambo hili lisimame mpaka tathimini ya mazingira itakapofanyika. Tunakwenda kupotea njia kabisa ya kukuza utalii. Mheshimiwa Spika hebu litizameni hili kwa upana wake.”

Zitto amshukia Kigwangalla Zitto amshukia Kigwangalla Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: