Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amemtaka
Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuisaidia Serikali kujenga utamaduni wa kuheshimu
sheria zinazopitishwa na Bunge
Akizungumza bungeni leo Mei 22, 2018 katika
mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2018/19, Nape amesema
wakati wakikamilisha kuandaa taarifa ya kamati kuhusu bajeti hiyo, Wakala
Huduma za Misitu Tanzania (TFS) walitangaza zabuni ya kukata miti katika pori
la Selous
Amesema ukubwa waliotangaza miti
itakapokatwa ni kama ukubwa wa Jiji la Dar es Salaam na wapo wanaosema ukubwa
huo unalingana na kisiwa cha Unguja, Zanzibar
Amesema hifadhi hiyo ni kubwa nchini na
kutangazwa kwa tenda hiyo kumeshtua
Hata hivyo, amesema sheria ya
usimamizi wa mazingira sehemu ya saba inatamka kuwa maeneo yatakayogundulika
kuwa na madini na maji kufanyiwa tathmini ya mazingira kabla ya mradi
kufanyika, lakini TFS imetangaza zabuni hiyo wakati tathmini
haijakamilika
Amesema tathmini hiyo ni muhimu kwa utambuzi
wa hali halisi ya mazingira na jamii inayozunguka eneo husika:
“Mwanasheria
Mkuu wa Serikali aisaidie Serikali kujenga utamaduni wa kuheshimu na kwa
unyenyekevu mkubwa naomba isitishe zoezi isubiri kwanza tathmini ya kimkakati
ya kimazingira.”
Amesema msitu huo unazunguka na mikoa mitano
ya Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma na kwamba haiwezekani kupuuza jambo
hilo.
Nape aitaka Serikali kuheshimu sheria
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment