|
Waziri wa Nishati, Dk Medard
Kalemani amesema mbio za kutatua kero za wananchi kuhusu matumizi mbalimbali
ya nishati ikiwamo ya kupikia sasa zimeanza rasmi
Dk Medard ambaye pia ni Mbunge wa
Chato ametoa kauli hiyo leo, Jumapili Mei 20, 2018, wakati akizindua ujenzi
wa miundombinu ya kuunganisha bomba la gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar es
Salaam
Uzinduzi huo ulifanyika Ubungo
jijini hapa na unatarajia kukamilika Septemba mwaka huu.
Kadhalika bomba hilo la gesi
litawaunganisha wananchi 1,000 wa mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara
watakaonufaika na gesi hiyo
“Leo nazindua, lakini kazi kubwa
ni utekelezaji na kuwafikishia miundombinu Watanzania ili wapate manufaa ya
matumizi ya rasilimali hii ya gesi,” amesema Dk Kalemani
Amesema ujenzi wa miundombinu hiyo
utagharimu Sh 4bilioni kwa awamu ya kwanza na maeneo yatakayonufaika ni
Mikocheni, Ubungo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sinza, Shekilango na Makongo
Juu
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Mhandisi Kapuulya Musomba
amesema hivi sasa wanafanya usanifu ili kujua watu wangapi watapata huduma ya
gesi kwa upande wa Dar es Salaam
|
|
Waziri wa Nishati asema mbio zimeanza rasmi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment