Waziri Mpango awajibu wabunge bajeti ya Ulinzi


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema si rahisi bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kutowekewa ukomo

Akijibu hoja za wabunge Mei 14, 2018 waliochangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2018/19, Dk Mpango amesema

“Kuna ushauri ulitolewa wizara isiwekewe ukomo hili si rahisi, fedha hazitoshelezi yako mahitaji mengi ambayo ni muhimu ambayo ninyi  wabunge mliyasemea kwa nguvu.”

“Mlisema maji, vifaa tiba, kilimo kuwa kwenye mtungi mmoja lazima uchukue kidogo,” amesema

Dk Mpango amesema Serikali itaendelea kuliwezesha jeshi kwa kadri rasilimali zinavyoruhusu

Amesema hadi Aprili, 2018 Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilikuwa limepata fedha za matumizi ya kawaida Sh307.9 bilioni

Waziri Mpango awajibu wabunge bajeti ya Ulinzi Waziri Mpango awajibu wabunge bajeti ya Ulinzi Reviewed by KUSAGANEWS on May 14, 2018 Rating: 5

No comments: