Waziri Jafo Atilia shaka thamani ya fedha ujenzi jengo la Maabara


Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh.Selemani Jafo ameikataa taarifa ya fedha iliyotumika katika ujenzi wa jengo la maabara katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mjini Mafinga kwa ufadhili wa mradi wa boresha afya USAID baada ya kuelezwa kuwa jengo hilo litagharimu zaidi ya Shilingi Milioni 990 kwa madai kuwa thamani ya fedha hailingani na uhalisia

Akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi mji wa Mafinga mkoani Iringa Waziri Jafo amesema kiasi cha Shilingi Milioni 990 kinatia shaka ikilinganishwa na jengo jingine la vyumba vitatu vya upasuaji lilojengwa hospitalini hapo kwa Milioni 232 kwa ufadhili wa nchi ya Japani

Jafo pia amemuagiza mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliamu kutowapeleka viongozi wa kitaifa katika jengo hilo mpaka watakapo patiwa thamani halisi kwa kuwa halmashauri imekuwa haishirikishwi katika hatua mbalimbali za ujenzi

Akiwa mjini Mafinga Jafo amekagua miradi inayoendelea kujengwa inayopatiwa fedha na wizara ya TAMISEMI ya ujenzi wa mabweni na vyumba vya madarasa shule ya sekondari Changarawe, ujenzi wa chumba cha upasuaji kituo cha afya Ihongole na madarasa mabweni na bwalo katika shule ya msingi makalala ya watoto wenye ulemavu mchanganyiko wanaofikia 554 kwa idadi

Waziri Jafo Atilia shaka thamani ya fedha ujenzi jengo la Maabara Waziri Jafo Atilia shaka thamani ya fedha ujenzi jengo la Maabara   Reviewed by KUSAGANEWS on May 26, 2018 Rating: 5

No comments: