Serikali imerasimisha eneo la Dovya
lililoko Boko kata ya Bunju maarufu kwa Somji lenye ukubwa wa ekari 366 kuwa
eneo la makazi.
Akitoa maelezo hayo leo Waziri wa
Ardhi Nyumba na Makazi William Lukuvi amesema wakazi wote waliovamia eneo hilo
mali ya serikali, hawatavunjiwa bali watahakikisha linapimwa na kila mtu
analipa kodi
"Nimekuja kumaliza mgogoro eneo
hili mali ya serikali niseme wote mliojenga ni wavamizi hamtavunjiwa litapimwa
na kila mtu atalipa kodi." Amesema Lukuvi
Amesema eneo hilo lililokuwa mali ya
Somji mwaka mpaka 1952, lakini baadaye serikali ililichukua hilo kwa
manufaa ya umma na kutaka kuwapangia wananchi namna ya kuishi ila wananchi
walikuwa na haraka na kuvamia eneo hilo
"Serikali ilitaka kuwapangia
namna ya kuitumia ardhi hiyo ila nyie mkawa na haraka ya kujipangia nimewahi
kuwa mkuu wa mkoa eneo hili nalifahamu lakini leo nimekuja niwaambie
ukweli," amesema
Waziri atatua mgogoro wa ardhi kwa Somji
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 12, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 12, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment