Mafuta ya kula Dar bado kizungumkuti


Zikiwa zimepita siku tatu tangu Serikali ilipowaagiza wafanyabiashara wa mafuta ya uto (kula) kuanza kuyaingiza sokoni, hali ya upatikanaji wake siyo nzuri kutokana na kuendelea kupanda bei jijini Dar es Salaam.
Leo ndiyo siku ya mwisho tangu Serikali ilipotoa amri hiyo na kuanzia kesho huenda msako katika bohari na maghala ya wafanyabiashara hao ukaanza

Akizungumza bungeni juzi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa muda wa hadi leo kwa wamiliki hao kuingiza sokoni bidhaa hiyo na kuonya kuwa iwapo hilo halitafanyika Serikali itaanza msako hu

Jana, Mwananchi lilipita katika maeneo mbalimbali ya

wafanyabiashara wa mafuta wa jumla na rejareja jijini Dar es Salaam ambap wengine walisema wamelazimika kuacha kuyauza na wale wanaoendelea nayo wamekuwa wakiyauza kwa bei ya juu
Wale wanaositisha uuzaji huo walisema wanafanya hivyo kutokana na hofu ya kukosa wateja kutokana na kuuziwa kwa bei ya juu na wauzaji
wakubwa itakayowalazimu na wao kupandisha bei
“Sijaweka mafuta ya uto hapa kwangu hii ni wiki sasa, hapo awali
nilikuwa ninanunua dumu la lita 20 Sh54,000 ghafla ikapanda hadi Sh56,000 nikaamua kuacha kwa sababu nawafahamu wateja wa mtaa huu nikipandisha bei hawatanunua,” alisema Joyce Pius, mmoja wa wafanyabiashara hao.

Joyce alisema kutokana na kutouza mafuta hayo dukani kwake anakosa wateja wa bidhaa nyingine kama vile unga wa sembe, ngano, mchele na sukari

Mfanyabiashara wa duka la jumla katika eneo maarufu la Kinondoni TX, Ally Salim alisema wakati mafuta yanapanda alikuwa na akiba ya kutosha kwenye ghala lao

Aliongeza kuwa kwa sasa wananunua lita 10 ya mafuta hayo kwa Sh38,000 na kulazimika kuuza kwa kati ya Sh40,000 hadi Sh42,000 kulingana na umbali wanakoyanunua

Mfanyabiashara wa duka la rejareja katika Kata ya Mzimuni, Lucy Lazaro alisema, “Nimenunua leo dumu la lita 20 kwa Sh64,000 kutoka Sh54,000 niliyonunua mwishoni mwa wiki iliyopita

“Tunalazimika kuuza chupa ya lita moja kwa Sh3500 hadi Sh400 kutoka Sh3200 ya awali na bado inakata. Hili dumu la lita 20 lina chupa za lita moja 20 tu, ukijumlisha kumwagika na kuwaongeza kidogo wateja unajikuta unabaki na chupa 18 na nusu au 19, hivyo ni hasara tu.”

Katika eneo la Temeke, mafuta ya kula nusu chupa yaliyokuwa yakiuzwa Sh500 sasa yanauzwa Sh700

Mchuuzi wa mafuta na bidhaa nyingine katika eneo la Tandika Azimio, Abdul Hafidh alisema anafanya biashara hiyo kwa mazoea. “Kupitia mafuta nitauza unga wa ngano na dengu, mchele na sukari kwa sababu wateja wangu ni wauzaji wa vitumbua na mama lishe, hivyo nisipokuwa na mafuta ya kula na walizoa kununua hapa nitawapoteza, ”alisema Hafidh
 Wasambazaji wakubwa

Gazeti hili jana lilifika katika ofisi za kampuni Murzah Oil Mills zilizopo eneo la Kipawa kutaka kujua kama agizo la Waziri Mkuu limeanza kutekelezwa, lakini lilipokewa na walinzi waliolekeza kuonana na ofisa mmoja aliyetoa maelezo kuwa si msemaji na kutaka atafutwe msemaji ambaye ilielezwa yupo katika ofisi nyingine zilipo eneo la Masaki

“Naomba chukua namba hii ya msaidizi wake (wa bosi) ili uzungumze naye,” alisema ofisa huyo ambaye hakutaka kujitambulisha

Hata hivyo, alipopigiwa msaidizi huyo alipokea na kutaka apewe muda ili awasiliane na bosi wake na kuahidi kutoa majibu baadaye. Hata hivyo, alipotafutwa tena simu yake iliita bila majibu yoyote

Juhudi za kuwapata wasambazaji wengine wakubwa wa mafuta hazikuzaa matunda



Mafuta ya kula Dar bado kizungumkuti Mafuta ya kula Dar bado kizungumkuti Reviewed by KUSAGANEWS on May 12, 2018 Rating: 5

No comments: