Watumishi wawili wa ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Arusha
wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru wakituhumiwa kwa mashtaka
mawili, likiwemo la kumvua nguo na kumpiga picha za utupu mwandishi wa habari
wa kujitegemea mkoani humo, Lucas Myovela
Watumishi waliofikishwa mahakamani leo Jumatano Mei 23, 2018
ni Swalehe Mwindadi ambaye ni ofisa itifaki katika ofisi hiyo na Amina Mshana
wa kitengo cha masjala
Awali, washtakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo saa tatu
asubuhi Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Patricia Kisinda, mwendesha mashtaka
wa Serikali, Sabina Silayo ameieleza mahakama kuwa washtakiwa wanakabiliwa na
mashtaka mawili
Amesema shtaka la kwanza ni kufanya unyang’anyi wa kutumia
silaha kinyume na kifungu cha 287A cha sheria ya kanuni ya adhabu, kifungu
kidogo cha 16 kilichorekebishwa mwaka 2002.
Silayo amebainisha kuwa Mei 13, 2018 katika eneo ya Sakina
jijini Arusha, washtakiwa hao kwa pamoja walimuimbia Myovela simu mbili za
mkononi na Sh75,000.
Amesema katika kosa hilo, washtakiwa hao kwa pamoja
walihamisha Sh9,500 kwa njia ya mtandao wa simu kabla ya kutekeleza jambo hilo
wakitumia panga na mkanda wa plastiki kumtishia mwandishi huyo
Mwendesha mashtaka amesema katika shtaka la pili, watuhumiwa
walifanya ukatili na udhalilishaji kinyume na kifungu cha 138 A cha sheria ya
kanuni za adhabu, kifungu kidogo cha 16 kilichorekebishwa mwaka 2002
Amesema siku hiyo katika eneo hilohilo washtakiwa hao
walimvua nguo Myovela na kisha kumpiga picha za utupu
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa hao walikana na
Silayo kuomba tarehe ya kutajwa kesi hiyo kwa kuwa upepelezi bado haujakamilika
Hata hivyo, Hakimu Kisinda aliamuru washtakiwa hao kupelekwa
mahabusu katika Gereza Kuu la Kisongo kwa kuwa kosa la kwanza linalowakabili
halina dhamana na kuahirisha kesi hiyo hadi Juni 6, 2018
NJE YA MAHAKAMA
Katika hali isiyo ya kawaida
Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali walifurika katika viunga vya mahakama
hiyo kushuhudia kesi ya mwenzao aliyefanyiwa ukatili huo na udhalilishaji.
Waliomteka na kumtesa mwandishi wa habari Wasomewa mashtaka mawili
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 23, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 23, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment