“MAAFISA HABARI WA MIKOA NA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUWENI WABUNIFU ILI KULETA MAGEUZI KATIKA SEKTA YA HABARI KATIKA TAIFA LETU”

Na Fatuma S. Ibrahimu - Arusha
 
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Habari Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dakta. Hassan Abbas  alipokuwa akiwamegea Maafisa Habari wa Mkoa pamoja na Jiji la Arusha  siri kuu Nne (4) za mafanikio katika kuleta mageuzi katika sekta ya Habari Serikalini. 

Ameyasema hayo alipowatembelea Maafisa Habari wa Mkoa pamoja na Jiji la Arusha mapema hapo jana katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambapo lengo kuu la ziara hiyo ilikuwa ni  kubaini changamoto mbalimbali zinazowakumba maafisa habari hapa nchini.

Siri nyingine tatu ni pamoja na kuwa washauri na wasemaji wakuu washughuli zinazofanyika katika maeneo yao ya kazi, kujali muda pamoja na ushirikiano baina ya maafisa husika.

“Kada ya habari ni muhimili mkubwa wa taifa hili hivyo wanahabari wote katika ngazi ya serikali mnapaswa kuisimamia kada hii  kwa weledi na kujituma kwa hali na mali na mtambue nafasi zenu zina mchango mkuwa kwa serikali  katika kupeleka taarifa sahihi kwa wananchi” alisema Dakta. Abbas.  

Aliongeza kuwa, kada ya Habari Serikalini iwe chachu ya kusaidia kutangaza na kutetea mageuzi mbalimbali yanayoendelea hapa nchini chini ya serikali ya awamu ya Tano.

Katika zara yake hiyo Dakta. Abbas aliambatana na uongozi mzima wa Chama cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali (TAGCO) ambapo mkakati huo wa idara ya Habari Maelezo na  Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali ni endelevu katika  Mikoa na Halmashauri zote hapa nchini.
MWISHO.




“MAAFISA HABARI WA MIKOA NA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUWENI WABUNIFU ILI KULETA MAGEUZI KATIKA SEKTA YA HABARI KATIKA TAIFA LETU” “MAAFISA HABARI WA MIKOA NA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUWENI WABUNIFU ILI KULETA MAGEUZI KATIKA SEKTA YA HABARI KATIKA TAIFA LETU” Reviewed by KUSAGANEWS on May 23, 2018 Rating: 5

No comments: