Walimu
waliotoka shule za sekondari na kwenda kufundisha msingi wametakiwa kutokuwa na
hofu kwa kuwa hakuna aliyeshushwa cheo na wachukulie ni kama mabadiliko ya
kawaida ya kituo cha kazi
Hayo yamesemwa
leo Mei 19 na Ofisa elimu mkoa wa Dar es Salaam, Hamisi Lissu alipokuwa
akifunga mafunzo ya kuwaweka sawa walimu wa shule za sekondari wanaoenda
kufundisha shule za msingi masomo ya sanaa
“Pamoja na
changamoto mnazokumbana nazo hamtakiwi kuwa na hofu kwani mabadiliko
mnayokutana nayo ni yakawaida kama kubadili kituo cha kazi,”amesema Lissu
Amesema hamasa
imeongezeka na hicho ni kiashirio tosha cha utendaji wao na atahakikisha
anatembelea vituo vyao ili kujua changamoto zao kwa kuwa wamekubali agizo la
serikali
Kwa upande
wake, Meneja mafunzo ya muda mfupi (Aden) Bungendi Joseph amesema walimu
wanaotoka sekondari kwenda msingi wanakumbana na changamoto ikiwemo kubadilika
kwa lugha,mazingira ya kazi pamoja kubadilika kwa mitaala
“Walimu hawa
mazingira wanayoenda ni tofauti hivyo tunawafundisha mazingira ya kulea
watoto,namna ya kufundisha lakini kikubwa ni mitaala inayojali umahiri”amesema
Bungendi
Advelina
Semakamba, Mwalimu wa Sekondari anayekwenda kufundisha shule ya msingi, amesema
alipopata taarifa alishtuka lakini baada ya kupata mafunzo ana imani
atakwenda kumudu kufundisha
Walimu watakiwa kuondoa hofu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 19, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 19, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment