Ni kama vile
Serikali imetumia mtindo wa kung'ata kupuliza baada ya kutangaza kushuka
kwa bei ya kununua pamba msimu huu na papo hapo kutangaza kufuta deni la zaidi
ya Sh30 bilioni kwa wakulima wa zao hilo linalolimwa katika mikoa 17 nchini
Bei mpya ya
Sh1, 100 kwa kilo imetangazwa leo Mesi Mosi na Waziri wa Kilimo Dk
Charles Tizeba wakati wa hafla ya uzinduzi wa msimu wa ununuzi uliofanyika
katika kijiji cha Bukama wilayani Igunga, ni pungufu kwa Sh100 ukilinganisha na
bei ya Sh 1, 200 ya msimu uliopita
Wakiwa bado
wanajitafakari kuhusu bei mpya, wakulima waliohudhuria uzinduzi walilipuka kwa
shangwe baada ya Dk Tizeba kutangaza neema ya Serikali kufuta deni la zaidi ya
Sh30 bilioni kwa wakulima hao lililotokana na mkopo wa viuatilifu
"Bei ya
pamba imeshuka kutokana na kuyumba kwa bei katika soko la dunia," amesema
Dk Tizeba
Amesema ili
kuwapunguzia gharama wakulima, Serikali imeamua kuwasamehe wakulima mkopo wa
viuatilifu na sasa watalipa mkopo wa mbegu pekee
Kwa mujibu wa
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba (TCB), Marco Mtunga, zaidi ya kilogramu 600
milioni zinatarajiwa kuvunwa msimu huu kutoka kwenye ekari milioni tatu
zilizolimwa na wakulima zaidi ya 500, 000 kutoka mikoa 17 na wilaya 54
zinazolima pamba
Kuhusu
mikakati ya msimu ujao wa Kilimo, Dk Tizeba alisema Serikali itasambaza bure
mbegu na viuatilifu na kuimarisha huduma ya ugani kwa wakulima ili kuongeza
tija
Wakulima pamba wafutiwa deni la Sh30 bilioni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment