VIDEO:SWALI LA 1 LA SUGU BUNGENI BAADA YA KUTOKA GEREZANI

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) ameitaka Serikali kuangalia upya baadhi ya sheria zake kwani ni mbovu na hazifai kutumika kwa sasa Sugu aliuliza swali la nyongeza bungeni leo Mei 21 na kusema kuwa kuna sheria ikiwemo sheria ya vyombo vya 
habari ambazo zinakwenda kinyume na katiba ya nchi ibara ya 18

 “Mfano mimi nilif ungwa kutokana na kuzungumza na wananchi wangu kuhusu watu kupigwa risasi, kuokota maiti kwenye viroba na demokrasia ya nchi,” amesema Sugu 

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa amesema kuwa sheria zote hupangwa na Bunge hivyo akasema maadam mbunge huyo amerudi bungeni basi iko haja ya kukutana na kujadiliana kuona namna ya kurekebisha "Kwanza nikukaribishe sana hapa bungeni, karibu sana mheshimiwa Mbilinyi," amesema Kuandikwa
VIDEO:SWALI LA 1 LA SUGU BUNGENI BAADA YA KUTOKA GEREZANI VIDEO:SWALI LA 1 LA SUGU BUNGENI BAADA YA KUTOKA GEREZANI Reviewed by KUSAGANEWS on May 21, 2018 Rating: 5

No comments: