Uchinjaji holela wapigwa marufuku Tunduru


Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imepiga marufuku uchinjaji wa mifugo katika machinjio na minada isiyo  rasmi ili kuwalinda walaji na magonjwa ya ulaji wa mifugo isiyopimwa na daktari lakini pia kuiingizia kipato halmashauri hiyo

Marufuku hiyo impigwa na Daktari wa Mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Dkt. Erick Kaisy aliyemwakilisha  Mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwenye uzinduzi wa awali wa mnada wa mifugo wa halmashauri hiyo ulioko Muhuwesi wilayani Tunduru unaotarajiwa kusaidia mikoa jirani ya Lindi na Mtwara. 

Kwa upande wao wafugaji wanauzungumzia mnada huo huku wakiiomba serikali kuendelea kuwaelimisha wafugaji waachane na kuuza Ngo'mbe zikiwa zizini na badala yake wazilete mnadani. 

Nao wafanyabiashara wa nyama ya Ngo'mbe wilayani Tunduru wanasema kuwa mnada huo utawasaidia  kwa kuwa awali walikuwa  wakifuata Ngo'mbe nje ya mkoa wa Ruvuma na hivyo unatarajiwa kusaidia kupunguza gharama ya nyama
Uchinjaji holela wapigwa marufuku Tunduru Uchinjaji holela wapigwa marufuku Tunduru Reviewed by KUSAGANEWS on May 26, 2018 Rating: 5

No comments: