Serikali yaombwa kumalizia ujenzi wa zahanat i mkoani Mtwara.


Wakazi wa kijiji cha Mngoji kata ya Madimba mkoani Mtwara wameiomba serikali na wadau wengine wa mendeleo kusaidia kumalizia ujenzi wa zahanati ambayo ipo katika hatua za kupaua, ili waondokane na adha ya akina mama

Wakazi hao wamesema kujengwa kwa zahanati hiyo kutasaidia wakazi wa kijiji hicho cha Mngoji wapatao 2,800 kupata huduma za afya kwa karibu zaidi, pamoja na kitongoji cha Uyuvi ambacho kipo umbali wa kilometa 10 toka zahanati ya Madimba

Akikabidhi msaada wa hundi ya mfano ya shilingi Milioni ishirini na moja laki moja hamsini na moja elfu na mia tano – 21,151,500 kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwa mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda ambae nae aliikabidhi kwa uongozi wa kijiji, meneja wa mawasiliano wa shirika la maendeleo ya Petrol – TPDC Mariam Mselemu amesema, shirika hilo limetoa msaada huo katika kutekeleza sera ya uwajibikaji kwa jamii ya kurudisha kidogo walichonacho kwa jamii. 

Kwa upande wake, mkuu wa wilaya Evod Mmanda mbali na kutaka fedha hizo zitumike kwa makusudi yaliyokusudiwa amewataka wananchi kuwa na taadhari kubwa ya ugonjwa wa Ebola kwa kuzingatia kijiji hicho cha mngoji ni miongoni mwa vijiji lilivyopakana na nchi jirani ya msumbiji

Serikali yaombwa kumalizia ujenzi wa zahanat i mkoani Mtwara. Serikali yaombwa kumalizia ujenzi wa zahanat i mkoani Mtwara.    Reviewed by KUSAGANEWS on May 26, 2018 Rating: 5

No comments: