TMA yatoa tahadhari ya mvua


Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa tahadhari ya kunyesha mvua kubwa juu ya wastani, kwa siku tano zinazoweza kusababisha mafuriko katika maeneo mengi nchini 

Kwa mujibu wa TMA, mvua hizo zitaanza leo Mei Mosi mpaka Mei 5 mwaka huu na zinatarajiwa kunyesha mikoa ya Dar es Salaam, 

Pwani, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba
Mikoa mingine ni Mara, Mara, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Katavi, Kigoma, Arusha, Kilimanjaro na Manyara

TMA imesema kiwango cha athari zinazoweza kutokea katika jamii ni pamoja na adha ya usafiri, barabara kubwa kutopitika na maji kujaa au kupita kwa kasi

Pia imetoa wito kwa wakazi wa maeneo ya mabondeni kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zitakazotolewa.
TMA yatoa tahadhari ya mvua TMA yatoa tahadhari ya mvua Reviewed by KUSAGANEWS on May 01, 2018 Rating: 5

No comments: