Kenyatta aongeza mishahara Kenya


Kenya. Rais Uhuru Kenyatta ametangaza nyongeza ya asilimia tano kwa kiwango cha chini cha mshahara nchini Kenya.Huku akisisitiza uwepo wa mazungumzo kutatua migogoro ya migomo

Nyongeza hiyo ya mishahara imetangazwa na Waziri wa Kazi Balozi Ukur Yatani Kanacho aliyemwakilisha Rais  Kenyatta wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani

Maadhimisho hayo ambayo yamefanyika kwenye viwanja Uhuru Park pia yamehudhuriwa na viongozi wengine mashuhuri kutoka serikalini
Mwaka 2017 Rais Kenyatta alihudhuria na kuhutubia taifa lakini mwaka huu 2018 mambo yamekuwa tofauti ambapo Waziri Yatani ndiye amemwakilisha kiongozi huyo

Kwa mujibu wa  hotuba ya Rais iliyosomwa na waziri huyo,  Serikali imetangaza kuwaongezea watumishi wa umma nyongeza ya asilimia tano ya mshahara.

 Hotuba hiyo imelenga  mambo manne yakiwamo  kuangazia usalama wa chakula nchini, makazi bora na nafuu, ujenzi wa viwanda ili kukabiliana na ukosefu wa ajira hasa kwa vijana, na matibabu bora

Kenyatta mwaka 2017 alitangaza nyongeza ya asilimia 18 kwa wafanyakazi wa umma

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Cotu Francis Atwoli amesema agizo hilo halijatekelezwa kwa baadhi ya kampuni na taasisi

"Kuna kampuni nyingi hazijatekeleza agizo hilo. Rais pia alipendekeza ushuru kwa wanaopokea mshahara wa chini ya Sh100,000 upunguzwe lakini hayo yote hayajazingatiwa," amesema  Atwoli

Kiongozi wa  upinzani Raila Odinga aliyehudhuria maadhimisho hayo, amesema  mkataba wa salamu zake na Rais Uhuru Kenyatta wa Machi 2018, ulilenga kuimarisha maisha ya Wakenya

"Mazungumzo yetu yaliegemea kuimarisha maisha ya wananchi wote, kwa msingi wa bidhaa na kodi nafuu ya nyumba," amesema  Odinga

Ameongeza  kuwa Nasa imeungana na Serikali ya Jubilee ili kuangazia matatizo yanayowakumba Wakenya ikiwamo kukabiliana na kero za ufisadi

Wengine waliohudhuria maadhimisho hayo ni; Waziri wa Elimu Amina Mohamed, Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Peter Kimunya,  Musalia Mudavadi, Seneta wa Nairobi Johnson Sakaja, Mwakilishi wa Wanawake Kaunti ya Nairobi  Esther Passaris, mbunge maalum wa ODM na katibu wa KNUT Wilson Sossion na  viongozi wengine mashuhuri serikalini.
Kenyatta aongeza mishahara Kenya Kenyatta aongeza mishahara Kenya Reviewed by KUSAGANEWS on May 01, 2018 Rating: 5

No comments: