Familia yataja tarehe ya mazishi ya aliyeuawa na polisi Tarime


Familia ya marehemu, Suguta Chacha imesema mazishi ya ndugu yao yatafanyika Alhamisi ya Mei 3, 2018 kijiji cha Nyabitocho

Chacha alifariki mikononi mwa Polisi, usiku wa Aprili 27 mwaka huu

Akizungumza leo Mei Mosi, na waandishi wa habari katika kijiji cha Nyabitocho kata ya Mbogi wilayani hapa, mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini, John Heche ambaye ni kaka wa marehemu alisema  uamuzi wa familia kuzika mwili huo umekuja baada ya kuridhika na hatua za serikali katika tukio hilo

"Tumeridhika na hatua zilizochukuliwa na jeshi la polisi kwa kumtia hatiani mtuhumiwa, kumfikisha mahakamani na kusomewa shtaka la kuua, kama familia tumeona ni vyema tuutangazie umma kuwa kesho tutauchukua mwili wa marehemu na kuuleta nyumbani na kesho kutwa (Alhamisi Mei 3) tutamzika." amesema Heche

Familia yataja tarehe ya mazishi ya aliyeuawa na polisi Tarime Familia yataja tarehe ya mazishi ya aliyeuawa na polisi Tarime Reviewed by KUSAGANEWS on May 01, 2018 Rating: 5

No comments: