Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA)
imetoa tahadhari ya kunyesha mvua kubwa juu ya wastani kwa siku tano mfululizo
zinazoweza kusababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo nchini
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa
leo na TMA, mvua hizo zimeanza jana Mei Mosi na zitaendelea mpaka Mei tano
mwaka huu na zinatarajiwa kunyesha katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga
pamoja na visiwa vya Pemba na Unguja
Mikoa mingine itakayoathirika na
mvua hizo ni Mara, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Katavi,
Kigoma, Arusha, Kilimanjaro na Manyara
TMA imesema kiwango cha athari
zinazoweza kutokea ni pamoja na mafuriko katika baadhi ya maeneo na kuathiri
jamii, adha ya usafiri kwa barabara kubwa kutopitika
Kwa mujibu wa TMA athari za mvua
hizo ni kujaa kwa maji au yanayopita kwa kasi na kuhamishwa kwa watu kutoka
maeneo yaliyoathiriwa
TMA yatoa tahadhari mvua kubwa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment