Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,
Profesa Joyce Ndalichako ameagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Baraza la
Vyuo vya Ufundi (Nacte) kufanya mapitio upya ya nyenzo wanazotumia kukagulia
ubora wa vyuo
Profesa Ndalichako amesema vikibainika
havina ubora wavifungie mara moja hata kama ni vya Serikali.
Akijibu hoja za wabunge leo Mei 2, 2018 bungeni mjini Dodoma walipojadili bajeti ya wizara yake ya mwaka 2018/19 amesema kuna baadhi ya wabunge wamelalamikia kuhusu wahitimu wa vyuo kushindwa kuandika wasifu
“Nacte na TCU wamekuwa wakifungia vyuo vingi
sana, lakini tatizo badi lipo, kwa hiyo naviagiza vyombo vya udhibiti wa elimu
kufanyia mapitio upya ya nyenzo za ukaguzi ikiwemo sifa za walimu, mitihani
inayotolewa na usahihishaji wao,” amesema Profesa Ndalichako.
“Iwapo watabaini havikukidhi ubora
wavifungie bila kuogopa mtu yeyote hata kama vikiwa vya Serikali, vifungiwe.” Ameongeza
Waziri huyo amewaagiza maofisa elimu nchini
kusimamia kwa karibu ubora wa elimu katika shule zilizopo katika maeneo yao
huku akidai kitendo cha kumfukuza mwalimu mkuu na kumuacha ofisa elimu wa eneo
husika ni uonevu kwa sababu wao ndiyo wanapaswa kusimamia ubora wa elimu
“Utakuta ofisa elimu ana shule tano tu
lakini anashindwa kuzisimamia na Serikali haitakubali kuwa na viongozi mizigo,”
amesisitiza Waziri huyo
Waziri Ndalichako azipa kazi TCU, Nacte
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment