Taharuki yaibuka kwa
Marehemu Aliyefufuka na kumtokea Mkewe
HALI ya Taharuki imewakumba wakazi wa Kijiji cha Leto ,Mamsera wilaya
ya Rombo kufuatia tukio la Mkazi mmoja wa eneo hilo aliyekuwa
amefariki dunia miezi miwili iliyopita kuibuka ghafla nyumbani
kwake aelezwa kuwa amefufuka.
Marehemu huyo aliyetajwa kwa jina la Richard David
Tarimo(28)alifariki kifo cha kutatanisha Marchi 30 mwaka huu baada kula Nyama
aliyoletewa na kaka yake aitwaye Senzo David na baadae kuanza kujisikia vibaya
na kufariki dunia ghafla wakati akikimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Mke wa marehemu alitwaye Mery Richadi anaeleza kuwa siku ya mazishi ya
kijana huyo kuliibuka jambo la kushangaza kutokana na udongo uliochimbwa kwenye
kaburi hilo kutotoshea wakati wa kufukia ,ndipo padre aliyekuwa akiongoza misa
ya kumwombea marehemu alipohoji kwanini kaburi halijai ,ndipo baadhi
ya waombolezaji walipomjibu kuwa haliwezi kujaa kwa sababu marehemu
amechukuliwa kimazingara.
Wiki mbili baada ya marehemu kuzikwa amekuwa akimtokea mkewe barabarani
mara kwa mara na kumtaka afunge Novena kwani huko aliko anateseka.
Mery anasema kuwa Mey 20 mwaka huu Marehemu mumewe aliibuka ghafla
nyumbani kwake, jambo lililomshangaza na watu wengine na kuibua taharuki ya
aina yake baada ya kudaiwa kufufuka.
Akisimulia mkasa huo mzito, Mery david alidai kuwa kabla ya kuibuka kwa
marehemu mumewe,mara kadhaa amekuwa akimtokea sehemu mbalimbali pindi anapokuwa
peke yake na kumweleza kuwa afunge Novena siku tisa kwani huko aliko anaishi
kwa mateso makubwa.
‘’Niliamua kufunga Novena na baada ya kumaliza mfungo wa siku tisa
ndipo ghafla akatokea mchungaji mmoja ambaye sikuwa namfahamu na
kunieleza kuwa marehemu mume wako atarejea ‘’Amesema Katika Kaburi la Marehemu Kaburi
Alipozikwa Marehemu
Mamia ya wakazi wa kijiji hicho waliokuwa wamefurika nyumbani kwa marehemu alilizingira kaburi la marehemu huyo wakitaka lifukuliwe ili waangalie kilichozika baada ya marehemu kuonekana akiwa hali ndani ya miezi mitatu.
Baba mzazi
wa kijana aliyefufuka, Mzee David Kimario ameshangazwa hatua ya kurejea kwa mwanae
uraiani baada ya kudaiwa kufufuka baada ya kufa, ila amefurahi kumpata
tena kijana wake kwa sababu kifo chake kilikuwa cha utata na cha muda mfupi.
Ila anachotaka ni kujua mwanaye alikuwa wapi na alikuwa akifanya
nini na kwenye kaburi kulizikwa nini.
TAHARUKI YATANDA ROMBO BAADA YA MAREHEMU KUFUFUKA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment