Spika asema bora liende


Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa mara nyingine jana alipinga majibu ya swali lililohusu sukari ambalo liliulizwa kwa mara ya pili  na mbunge, akisema kuwa bado halijajibiwa
Swali hilo liliulizwa na Mbunge wa Baraza la Wawakilishi Jaku Ayoub Hashim

Hashim aliuliza swali hilo  leo Mei 18 bungeni baada ya kuwa liliulizwa mwanzoni mwa mwezi na serikal kutakiwa kulitolea ufafanuzi

Hashim alihoji, kuna tatizo gani linalofanya sukari iuzwe bei ya juu kwa upande wa Tanzania bara kuliko Zanzibar na akahoji Serikali inachukua hatua gani kukomesha tatizo hilo?

Jaku pia amesema kwa upande wa Zanzibar kipindi ambacho matumizi ya sukari kwa wananchi yanaongezeka, Serikali inashusha ushuru wa kuingiza sukari nchini akahoji ni kwa nini Serikali isiige mfumo huo na kupeleka unafuu kwa wananchi wa bara?

Awali, swali hilo lilijibiwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage  na majibu yake yalizua utata hadi Spika Ndugai akaagiza Serikali kutafuna namna ya kulitolea ufafanuzi suala  hilo. Pia aliagiza swali hilo kurudiwa upya ili mbunge apate majibu yanayojitosheleza

Serikali kupitia Waziri Mwijage ilipeleka majibu bungeni na kulitolea ufafanuzi jambo hilo ambalo hata hivyo bado lilikuwa na sintofahamu kwa wabunge

Jana, Serikali ilipeleka majibu ya swali hilo ambayo yalijibiwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Stella Manyanya lakini Ndugai akasema halijajibiwa kulingana na muuliza swali alichotaka

“Ujue waheshimiwa wabunge swali hili halijapata majibu kabisa, maana ukiangalia lilivyoulizwa na majibu yake yalivyotolewa utaona vitu viwili tofauti, lakini nalimaliza kwa namna hiyo, haya tunasonga mbele,” amesema Ndugai

Akijibu swali hilo, Manyanya amesema bei ya sukari kwa gunia la kilo 50 ni Sh 101,000 hadi Sh 105,000 kwa Dar es Salaam na Sh 71,000 hadi 77,000 kwa Zanzibar

“Mapitio ya bei hizo yanatokana na utozaji wa ushuru na kodi, na inaonekana dhahiri kuwa kiasi cha kodi kinachotozwa kwenye gharama za mfuko wa kilo 50 Zanzibar ni kidogo ukilinganisha na kodi inayotozwa kwa Dar es Salaam ambayo ni asilimia 25 na 18 vyote kwa pamoja,” amesema Manyanya
Spika asema bora liende Spika asema bora liende Reviewed by KUSAGANEWS on May 18, 2018 Rating: 5

No comments: