Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe amemwomba Spika
wa Bunge, Job Ndugai kuridhia kufanyika mabadiliko ya kanuni za Bunge ili
kuruhusu hoja zinazohusu wananchi zinazojitokeza ndani ya Bunge zisifie kwenye
vikao vya vyama ‘Party Caucus.’
Bashe amesema hayo bungeni leo Mei 18, 2018 wakati
akichangia bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018/19 ambapo ameitaka
Serikali kuiondoa bajeti hiyo na kwenda kujipanga upya kwani haijatoa dira ya kuwasaidia
wafugaji na wafuvi.
Akichangia huku Bunge likiwa kimya, Bashe amesema
atashangazwa na wabunge wa CCM kama wataipitisha bajeti hiyo na kuwataka
kuzingatia mkataba baina ya wananchi na CCM ambao waliwapigia kura
Bashe amesema kabla ya kuingia bungeni mwaka 1995, alipewa
kadi ya CCM; “Kwa hiyo mimi ni CCM kwanza kabla ya ubunge na muweke katika
rekodi.”
Amesema katiba ya CCM inazungumzia madhumuni ya kuanzishwa
chama hicho na inasisitiza kusimamia haki na maendeleo ya wakulima, wafanyakazi
na wananchi wengine wawanaofanya shughuli halali za kujitegemea na kuona kila
mtu ana haki ya kutaka malipo yanayotokana na kazi yake.
“Nimelisoma dhumuni
hili makusudi kabisa, ili Serikali wajiulize swali je wanatimiza wajibu wa wana
CCM milioni saba nane waliokaa katika foleni ili kuiweka madarakani.
“Mkataba uliopo kati
ya wananchi na Serikali ni CCM na sisi, wananchi wameipa dhamana CCM, juzi
tumepitisha bajeti (ya kilimo) na kwa masikitiko makubwa tutapitisha na hii,
ndio kawaida yetu,” amesema
Amesema bajeti ya kilimo katika fedha za maendeleo ilitoa
asilimia 18, katika bajeti ya mifugo na uvuvi haijapeleka fedha zozote huku
akikataa kuiunga mkono
Bashe amesema hoja binafsi iliyokuwa iwasilishwe na Mbunge
wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ilishindikana kuwasilishwa bungeni na kuitwa katika
kikao cha kamati ya uongozi, “Baada ya hapo tukaitwa (Nape na Bashe)
katika kikao cha chama na baadae ikaenda kufia huko, mheshimiwa spika tubadili
kanuni ili hoja zinazowahusu wananchi zisiende kufia katika vikao vya chama.”
Bashe ataka mabadiliko ya kanuni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 18, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 18, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment