Mwanafunzi wa darasa la nne wa shule ya msingi Sabasaba
jijini Mwanza, Dotto Baraka (13) amefariki dunia baada ya kulipukiwa na betri
ya simu aliyokuwa akiiunganisha na radio chakavu
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo Mei 18,
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea Mei
17 mtaa wa Igoma Mashariki jijini Mwanza
“Baada ya kutoka shuleni, marehemu akiwa na watoto wenzake
alianza kutengeneza radio chakavu kwa kuchukua betri ya simu na kuunganisha
kwenye nyanya za radio hiyo akitumia mdomo ndipo mlipuko ulipotokea na
kusababisha kifo chake," amesema Kamanda Msangi
Amesema mlipuko huo ulisambaratisha mdomo, taya, meno
na koo la marehemu aliyefia njiani wakati majirani wakijaribu kuokoa maisha
yake kwa kumkimbiza hospitali
Kamanda Msangi amesema wakati tukio hilo linatokea,
wazazi wa watoto hao walikuwa safarini, wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga
Amesema hakuna mtoto mwingine aliyejeruhiwa katika tukio
hilo.</p></div><div><p>
Kamanda Msangi amewaomba wazazi kuwa makini wanapowaacha
watoto majumbani wenyewe kwa kuwakanya kuepuka kuchezea vitu vinavyoweza
kuhatarisha maisha yao na mali
Mwili marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa wa
Mwanza, Sekou-toure kwa ajili ya uchunguzi zaidi kabla ya kukabidhiwa kwa
familia, kwa ajili ya mazishi
Mtoto afariki kwa kulipukiwa betri ya simu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 18, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment