Mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Tanzania bara (VPL) mwaka
2017/18, timu ya Simba leo wameliteka Bunge jijini Dodoma
Mabingwa hao pamoja na benchi la ufundi na viongozi
mbalimbali wa timu hiyo, wametembelea Bunge baada ya kupata mwaliko wa Spika
Job Ndugai
Hata kabla hawajatambulishwa na Mwenyekiti wa Bunge, Najma
Giga, Naibu Waziri wa Tamisemi, Joseph Kakunda alianzisha 'shangwe' bungeni
humo
Ilikuwa hivi, kabla ya Kakunda kujibu swali la Mbunge wa
Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige, Naibu Waziri huyo ameanza kwa kusema, leo
Mei 14, 2018 ameamka saa 10 alfajiri kujiandaa kujibu maswali lakini kubwa ni
furaha ya ubingwa
Huku wabunge wakishangilia, Kakunda akiwa mwenye furaha
akasema,"Sasa naamini Watanzania watapata wawakilishi wazuri wa michuano
ya kimataifa, hawatatupa presha."
Kakunda muda wote wa kujibu maswali ya wabunge amekuwa
akichombeza maneno ya furaha ya ubingwa wa Simba na uwapo wao bungeni
Hakuwa Kakunda pekee, bali hata Mbunge wa Ilala (CCM), Azzan
Zungu aliposimama kuuliza swali la kujua mikakati ya kuboresha michezo kwa
vijana na akaanza kwa kusema
"Humu ndani kaingia mnyama mkali sana, lakini tuko
salama," na shangwe kuendelea ukumbini
Mbunge wa Mpwapwa (CCM), George Lubereje naye kabla ya
kuuliza swali amewapongeza Simba akisema wamefanya kazi kubwa sana kuchukua
ubingwa hata kabla ligi haijaisha
Simba watinga bungeni, wawapa raha wabunge
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment