Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema
Nchimbi amegoma kukaa eneo alilotengewa mgeni rasmi kwa kile alichodai hawezi
kukaa kivulini wakati watoto wanakaa juani
Tukio hilo limetokea leo, Mei 14,
wakati Nchimbi akizindua wiki ya elimu inayofanyika kitaifa wilayani Mkalama
mkoani Singida
Nchimbi amechukua hatua hiyo baada
ya kupokea maandamano ya shule mbalimbali wilayani humo na kuona watoto wote wamesimama
juani
"Mimi ni mama, mimi ni
mwakilishi wa serikali siwezi kukaa kivulini halafu niwaangalie watoto wako
juani kwa hiyo watu wote wa meza kuu tushuke pale kwenye jua,”amesema
Ameongeza: "Serikali ya awamu
ya tano ina upendo na huruma kwa watoto na Watanzania haiwezekani watu wazima
wakae kivulini watoto wakae juani
Baada ya kauli hiyo watendaji,
viongozi wa serikali na wadau wa elimu ambao walikuwa wamekaa jukwaani walishuka
chini na kuhamishia viti vyao juani
Katika hafla hiyo Nchimbi alipokea
maandamano ya wanafunzi wakiwa na mabango mbalimbali yenye ujumbe kuhusu elimu
RC agoma kukaa kiti cha mgeni rasmi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment