Bajeti Wizara ya Ulinzi yawasilishwa

Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika mwaka wa fedha 2018/19 imeongezeka kutoka Sh 1.72 trilioni ya mwaka wa fedha 2017/18 na kufikia Sh 1.91 trilioni

Kati ya fedha hizo Sh 1.67 trilioni ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh 234 bilioni ni kwa ajili ya kugharamia shughuli za maendeleo

Akiwasilisha bajeti hiyo bungeni leo Mei 14, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi amesema wizara katika utekelezaji wa bajeti yake ya mwaka 2017/18 imekabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni upungufu wa rasilimali fedha

Amesema kiwango kilichoidhinishwa na bunge kilikuwa Sh 1.72 trilioni katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi ya Sh 3.2 trilioni

Aidha, amesema bajeti iliyoidhinishwa kwa upande wa fedha za maendeleo hutolewa kwa kiwango kidogo

“Hali hii imesababisha kulegalega kwa utoaji wa huduma na wizara kuendelea kuwa na madeni yanayoathiri utendaji wa wizara na kupoteza uaminifu kwa wazabuni wanaotoa huduma na kuleta bidhaa mbalimbali,” amesema

Dk Mwinyi amesema hadi kufikia Aprili mwaka huu, wizara ilikuwa imepokea Sh 181.58bilioni sawa na asilimia 82.91 bilioni kati ya Sh 219 bilioni zilizoidhinishwa na bunge katika bajeti ya 2017/18 kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo




Bajeti Wizara ya Ulinzi yawasilishwa Bajeti Wizara ya Ulinzi yawasilishwa Reviewed by KUSAGANEWS on May 14, 2018 Rating: 5

No comments: