Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, imewaona
washitakiwa sita kati ya saba katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Erasto
Msuya kuwa wana kesi ya kujibu
Mshitakiwa wa nne, Jalila Zuber ameachiwa
huru baada ya uamuzi wa Jaji Salma Maghimbi, kueleza kuwa ushahidi uliotolewa
na mashahidi wa upande wa mashitaka haukumgusa kiasi cha kufanya awe na kesi ya
kujibu. Jaji Maghimbi ametoa uamuzi huo leo Mei 14
Washitakiwa ambao wameonekana wana kesi ya
kujibu ni mshitakiwa wa kwanza, Sharifu Mohamed, mshitakiwa wa pili, Shaibu
Jumanne, mshitakiwa wa tatu, Mussa Mangu, mshitakiwa wa tano, Karim Kihundwa,
mshitakiwa wa sita, Sadick Jabir na mshitakiwa wa saba, Ally Majeshi
Mauaji ya Bilionea Msuya, mmoja aachiwa huru
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment