Mcheza filamu, Elizabeth Michael maarufu Lulu amebadilishwa
kifungo na sasa atatumikia adhabu hiyo akiwa nje yaani ‘kifungo cha nje’.
Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela Novemba mwaka
jana baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake,
Steven Kanumba
Akizungumza Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza, Lucas Mboje
amesema Lulu amebadilishiwa adhabu na atatumikia kifungo cha nje kwa amri
ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam
“Lulu amebadilishiwa adhabu na ameachiwa juzi Jumamosi kati
ya saa 2 hadi 3 asubuhi. Hii si kwamba ameachiwa huru, bali amebadilishiwa
adhabu na atatumikia kifungo chake nje, kitaalamu tunaita ‘community service’”
amesema Mboje
Lulu abadilishiwa adhabu, sasa kutumikia kifungo cha nje
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment