Wengi wetu tumezoea kuwaona watu wenye
matatizo ya akili wakiokota makopo majalalani, huku wengine wakiwekwa kwenye
maeneo maalumu kama vile hospitali kupatiwa matibabu
Hata hivyo, hayo ni tofauti na aliyojionea
mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye wakati
akitumikia kifungo cha miezi mitano jela katika Gereza Kuu la Ruanda mjini
hapa, anadai alishuhudia watu wa aina hiyo wakiwa ndani ya gereza hilo
wakitumikia vifungo vyao
Katika mwendelezo wa mahojiano na Mwananchi,
Sugu anasema akiwa kiongozi alitarajia kukutana na changamoto zinazowakabili
wafungwa kama vile za chakula, malazi, matibabu na msongamano gerezani
Pia anasema alitarajia kushuhudia changamoto
wanazokumbana nazo askari magereza, lakini hakutarajia kuona kuwa kuna nyingine
zaidi ya hizo
“Hayo niliyatarajia na nimeyakuta sema tu
sikujua kama mengine yapo kwa kiwango cha juu zaidi, sikujua kama Taifa hili
linashindwa hata kununua sare za wafungwa ili watoke nje wakafanye kazi,”
anasema
“Sikutarajia kama magereza nitakuta kuna
wafungwa ambao ni wagonjwa wa akili, vichaa, badala ya kupelekwa Mirembe
(mkoani Dodoma) na maeneo mengine unawakuta wamefungwa kwenye gereza letu lile.
Nilimkuta kijana mle ni mgonjwa wa akili, lakini amekaa gerezani tangu mwaka
2001.”
Mbunge huyo anasema hilo ni jambo ambalo
lilimshangaza ikizingatiwa kwamba watu hao wanastahili haki tofauti uraiani
zikiwamo za matibabu
“Kwa hiyo sikutarajia kuwakuta watu wenye matatizo ya akili wapo mle wamechanganywa na wafungwa wengine wa kawaida badala ya kupelekwa Mirembe wakapate msaada,” anasema Sugu
Anasema watu wenye matatizo hayo muda wote
wanakuwa wamekaa tu gerezani na hawafanyi kazi yoyote, lakini wanaendelea
kutumikia kifungo na kwamba, kazi yao ni kula na kulala tu
Sugu anasema kuna wafungwa wameingia
gerezani wakiwa ni wagonjwa, lakini wengine wamekumbwa na maradhi wakiwa ndani
ya gereza
Ajiita mtu mashuhuri
Anasema kitu kingine ambacho hakukitarajia
ni baada ya kutoka gerezani na kuona namna watu walivyompokea uraiani, jambo
ambalo limemfanya kwa sasa ajione kuwa mtu mashuhuri na si maarufu tena
“Nilichokitarajia ndicho nilichokutana na
nacho baada ya kutoka gerezani. Kabla ya kufungwa kwangu nilikuwa maarufu sana,
lakini baada ya hili kwa sasa nimekuwa mtu mashuhuri,” anasema mbunge huyo
“Awali nilikuwa naombwa kupiga picha na watu
mtaani nikipita kwa siku picha 10 hadi 20, lakini sasa hivi nikipita tu mtaani
kwa siku naombwa kupiga picha na watu hadi 100.”
Awalilia askari
Sugu anasema unapozumguzia shida za
gerezani, hazipo kwa wafungwa pekee, bali pia kwa askari anaodai kuwa wana hali
ngumu tofauti na watu wengine wanavyoweza kuwafikiria na kuwazungumzia
Anasema hali hiyo inawakosesha ari ya
kufanya kazi kwa moyo
“Shida hazipo tu kwa wafungwa, zipo kwa
askari magereza. Askari wana hali mbaya. Kwa hiyo hata mtu anaposema wale
wafungwa lazima wafanye kazi, si lazima wawepo watu wa kuwasimamia, sasa watu
hao hawana morali, “ anasema
“Askari amepandishwa cheo hadi nyota tatu na
miaka imepita, lakini cha kushangaza bado anaendelea kupokea mshahara wa nyota
moja, haujapanda.”
Sugu anasema sio kwamba sare ni tatizo kubwa
kwa wafungwa pekee, bali hata kwa askari na wapo wanaolazimika kujishonea nguo
zao jambo linalonatia doa nchi kushindwa kuwashonea sare nyingi
watakazobadilisha mara kwa mara. “Uniform (sare) kwa askari wenyewe ni shida.
Anasema zaidi askari hao wanachopewa ni vifungo pekee hivyo kinachofanyika ni askari kubadili vifungo kutoka kwenye nguo ya zamani na kuweka kwenye nguo nyingine atakayokuwa ameshona
“Zaidi wanachopewa ni vifungo tu vya chuma
na mwingine alipewa miaka minne iliyopita na kwa vile haviishi, hivyo sare yake
ikichakaa basi anatoa vifungo anakuja kuwekea nguo mpya,” anasema Sugu
“Na wengine inafikia nguo inachakaa
anapeleka kwa fundi na kichofanyika ni kubadilishwa nje inakuwa ndani na ndani
inakuwa nje na hii nimeishuhudia mwenyewe kwa kuwa mafundi wanaowatumia ni
wafungwa mlemle ndani.
Kwa hiyo unakuta askari anasema ‘eee!! bwana hebu
nipigie nje ndani’ kwa sababu inakuwa imepauka sana. Kwa hiyo inabadilishwa
pale inakuwa nguo mpya na mtu anaigonga pale anaendelea kuivaa
Sikutarajia kuwakuta wafungwa wenye ugonjwa wa akili gerezani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment