|
Woga wa kupoteza vyeo, kutojiandaa
na wivu, vimetajwa kuwa chanzo cha wataalam wengi kushindwa kuwaandaa
watu watakaorithi madaraka yao pindi wanapostaafu ama kuacha kazi
Akizungumza leo Mei 20 na
Wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji Majenzi, (AQRB) Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam (UDSM) Goodluck Urassa amesema sababu nyingine ni woga
wa mabadiliko
“Wengine wanaogopa kupoteza
ukubwa. Wewe ulikuwa ni CEO (Mkurugenzi Mkuu) watu wanakujua kabisa wewe ndio
mkubwa kumuachia mtu mwingine na wewe ukabaki hapo hapo unashindwa. Wengine
ni woga tu wa mabadiliko,
wengine wivu hataki mtu wa chini
apate, kuna watu hata watoto wao wanawaonea wivu,”amesema
Amezitaja njia za kufikia
mafanikio katika biashara ni pamoja na kumchagua mwanafamilia lakini kama
hakuna mtu wa kusaidia unaweza kuchukua mtu kutoka nje ya familia
Pia amesema kumtafuta meneja
mtaalam ama ikishindikana kuuza sehemu ya hisa za kampuni kwa mtu mwingine
Mwenyekiti wa Bodi ya Wabunifu
Majengo nchini, Dk Ludihija Bulamile amesema uamuzi wa Serikali wa
kutumia kwa kiasi kikubwa taasisi za Serikali katika ujenzi wa miradi ya umma
itaathiri sekta za umma na binafsi kwa kiasi kikubwa
“Hii ni kwa sababu sekta binafsi
inashiriki kwa kasi kubwa sana kufundisha vijana wanaomaliza vyuo vikuu ili
waweze kusajiliwa na bodi,”amesema
Amesema pia kampuni binafsi ndizo
zinazoajiri wataalam wengi wanaomaliza vyuo, hivyo uamuzi huo utawakosesha
mahali pa kujifunzia.
|
|
Profesa UDSM awapa neno wataalamu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment