Waziri wa Kilimo
Mhe. Dkt. Charles Tizeba, amefunguka kuwa hakutarajiwi kuwa na upungufu wa
sukari hapa nchini kwa sababu hadi kufikia tarehe 10 mei 2018 katika maghala ya
wazalishaji na wafanyabiashara kulikuwa na tani 78,147.67 za sukari na
kiasi kingine tani 25,441.25 zipo Bandarini.
Waziri Tizeba amesema Serikali
imeagiza sukari kiasi cha tani 70,354.35 kutoka nchi za nje lengo likiwa ni
kujipanga ili kuhakikisha kuwa hapatokei upungufu wa bidhaa hiyo hapa nchini.
Waziri Tizeba amefafanua kuwa
tani 60,539.35 ya sukari itaanza kuingia hapa nchini katikati ya mwezi
Mei 2018 ambapo kiasi kilichobaki cha tani 9,815 kitaingia mwezi June
mwaka
"Kwa kiasi cha sukari
ambacho tayari kipo hapa nchini kikijumlishwa na kiasi ambacho kitaingia
hivi karibuni kutoka nje ya nchi ni dhahiri kwamba nchi haiwezi kupata
upungufu wa bidhaa hiyo", alisema Mhe.Waziri.
Awali Dkt.Tizeba alisema kwamba mahitaji ya sukari nchi nzima ni tani 630,000 ambapo kati ya hizo, tani 145,000 ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani na tani 485,000 ni kwajili ya matumizi ya kawaida.
Awali Dkt.Tizeba alisema kwamba mahitaji ya sukari nchi nzima ni tani 630,000 ambapo kati ya hizo, tani 145,000 ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani na tani 485,000 ni kwajili ya matumizi ya kawaida.
Serikali yaweka wazi kuhusu upungufu wa sukari
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 13, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 13, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment