Sauti ndani ya kontena yazua taharuki bandarini

Mkazi wa Miembeni mjini Unguja, aliyetajwa kwa jina moja la Hassan amenusurika kifo baada ya kutolewa ndani ya kontena alikojifungia

Msimamizi wa makontena katika Bandari ya Malindi, Ibrahim Abdallah akizungumza amesema chanzo cha mtu huyo anayekadiriwa kuwa na miaka 30 kuingia kwenye kontena na kujifungia hakijajulikana

Amesema wakiwa katika kazi zao eneo hilo saa moja asubuhi walisikia sauti ikitoka ndani ya kontena lililo juu ya jingine hivyo kuzua taharuki miongoni mwao

Abdallah amesema sauti iliyosikika kutoka ndani ya kontena ilisema, “Nakufaaa.”

Amesema walipofika eneo hilo waliuliza, “wewe ni nani” na jibu walilopatiwa ni, “Hassan.”
"Baada ya kutaja jina tulifungua kontena ambalo alikuwa amelifunga na kumtoa akiwa na hali mbaya kiafya na tulimpeleka Hospitali ya Mnazi Mmoja ili kupatiwa huduma ya kwanza," amesema

Kuli katika bandari hiyo, Mohamed Khamis Makame amesema ni mara ya kwanza kutokea tukio hilo eneo hilo, hivyo amesema wanapaswa kuwa makini katika ulinzi
Sauti ndani ya kontena yazua taharuki bandarini Sauti ndani ya kontena yazua taharuki bandarini Reviewed by KUSAGANEWS on May 13, 2018 Rating: 5

No comments: