Papa amteua Padri Anthony Lagwen Askofu Jimbo la Mbulu


Baba Mtakatifu, Papa Francisko amemteua Padri Anthony Lagwen kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Mbulu

Taarifa iliyotolewa na leo na Makao Makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican imesema Askofu mteule Lagwen aliyepata daraja la upadri Oktoba 18, 1999,  alizaliwa  Julai 5, 1967 huko Tlawi, Jimboni Mbulu mkoani Manyara

Taarifa hiyo iliyokaririwa na Redio Vatican, imesema baada ya masomo yake ya msingi, aliendelea na masomo ya sekondari katika Seminari Ndogo ya Sanu, Jimbo Katoliki la Mbulu na baadaye akapata masomo ya falsafa kutoka Seminari kuu ya Ntungamo, iliyoko Jimbo Katoliki la Bukoba.

 Baada ya hatua hiyo alihamia katika Seminari Kuu ya Kipalapala, Jimbo Kuu la Tabora ili kuendelea na masomo ya kitaalimungu (Theolojia).

Tangu wakati huo, katika maisha na utume wake wa kipadri kuanzia mwaka 1999 hadi mwaka 2000, alikuwa Paroko-usu wa Parokia ya Bashay jimboni Mbulu. Kati ya mwaka 2000 hadi mwaka 2004 akapelekwa na Jimbo kujiendeleza zaidi katika masuala ya biashara kwenye Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Mwanza

Kati ya mwaka 2004 hadi mwaka 2009 akateuliwa kuwa mchumi wa Jimbo Katoliki la Mbulu. 

Kati ya mwaka 2009 hadi mwaka 2011 akatumwa tena na Jimbo kujiendeleza zaidi katika masuala ya biashara kwenye Taasisi ya East and Southern Africa Management Institute iliyoko Jijini, Arusha. 
Kuanzia mwaka 2012 hadi kuteuliwa kwake leo, amekuwa ni mchumi wa mali za Kanisa, Jimbo Katoliki la Mbulu.
Papa amteua Padri Anthony Lagwen Askofu Jimbo la Mbulu Papa amteua Padri Anthony Lagwen Askofu Jimbo la Mbulu Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: