Chuo Kikuu cha Mzumbe kimezindua kituo cha msaada wa
kisheria kwa ajili ya kuhudumia watu mbalimbali, wakiwamo wanaoishi vijijini
wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji ufumbuzi wa kisheria
Akizungumza leo Mei
22, 2018 Mkuu wa Kitivo cha Sheria chuoni hapo, Profesa Cyriacus Binamungu
baada ya kufanya uzinduzi wa kituo hicho cha Huduma ya Msaada wa Sheria,
amesema, “Serikali imekuwa mstari wa mbele kutetea wanyonge na kusisitiza haja
ya kulinda haki za wanyonge popote nchini.”
“Hivyo nasi kwa kutambua hilo tukaona kuanzisha kituo ili
kuwapatia huduma ya karibu watanzania. Wananchi wamekuwa wakisimamisha misafara
ya viongozi wa Serikali na kutoa malalamiko juu ya mambo kadhaa wanayoamini ni
kinyume na haki zao kwa kuwa wamekosa sehemu sahihi ya kutoa malalamiko na
kupata haki zao.”
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mohamed Utaly
amesema wanachi wengi wanashindwa kupata haki mahakamani kwa kukosa fedha,
uelewa mdogo wa masuala ya kisheria, hivyo kuanzishwa kwa kituo hicho kutaleta
manufaa kwa wananchi wa chini
“Ni wakati sasa wa wanataaluma kutumia taaluma yenu
kusaidia jamii inayowazunguka. Endeleeni kufanya utafiti na kujua nini hasa
wananchi wanahitaji katika masula ya kisheria ndani ya wilaya ya Mvomero na
Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuweza kuwasaidia wananchi,” amesema
Makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Lugano Kusiluka amesema
kuanzishwa kwa kituo hicho ni mpango mkakati wa wake wa kuhudumia jamii,
kila kitivo ndani ya chuo kinajiandaa kuhudumia jamii
Chuo Kikuu Mzumbe chazindua kituo cha msaada wa kisheria
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment